IQNA

Zaidi ya watu 200 wasilimu Imarati

12:36 - August 07, 2010
Habari ID: 1968273
Katika kipindi cha miezi miwili iliyopita watu 205 kutoka mataifa mbalimbali Wameikubali dini tukufu ya Kiislamu katika Umoja wa Falme za Kiarabu.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, Yusuf Saeed, Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Kiislamu cha Imarati amesema watu hao waliosilimu walikuwa wamekwenda Imarati kwa sababu mbalimbali zikiwemo za kibiashara na kitalii. Amesema watu hao wamevutiwa na Uislamu na baada ya kutafuta muongozo katika idara za kutoa maelezo kuhusu Uislamu, walikubali kusilimu.
Ameongeza kuwa vituo vya Kiislamu vya Imarati vijulikanavyo kama Darul Birr ndivyo ambavyo hutoa maelezo kuhusu Uislamu kwa kutumia mbinu za hekima. Amesema vituo hivyo vimefasiri vitabu vya Kiislamu na Qur'ani Tukufu kwa lugha za Kiingereza, Kichina, Kirussia, Kifaransa , Kiurdu na lugha nyiginezo zinazotumiwa na wanaosilimu. Ameongeza kuwa vitabu hivyo hutolewa kwa wanaohitajia na kwamba katika kipindi cha miezi miwili iliyopita, vituo hivyo vimesambaza vitabu elfu kumi katika maeneo mbalimbali ya Umoja wa Falme za Kiarabu.
627741
captcha