IQNA

Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu

Kisomo cha makarii Wairani ndani ya Masjidul Haram ni fahari kwa Iran ya Kiislamu

16:40 - December 07, 2010
Habari ID: 2043498
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema kuwa kisomo cha Qur'ani cha maqari wa Kiirani ndani ya Masjidul Haram ni fahari kubwa kwa Iran ya Kiislamu na akaongeza kuwa katika miaka ya hivi karibuni kumekuwepo harakati nzuri za kutilia maanani Qur'ani na kiraa yake katika siku za ibada ya hija.
Ayatullah Khamenei ameyasema hayo Jumatatu Desemba 6 katika mkutano wake na maafisa wa msafara wa hija wa Iran.
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa viongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran ni wabeba bendera ya umoja katika ulimwengu wa Kiislamu.
Ameashiria umuhimu wa kuwepo umoja wa Kiislamu na kusisitiza udharura wa kupunguzwa hitilafu kati ya Waislamu wa Shia na Suni. Amesema kuwa viongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu walikuwa vinara na wabeba bendera ya umoja na mshikamano katika ulimwengu wa Kiislamu hata kabla ya ushindi wa mapinduzi hayo.
Ayatullah Khamenei amewashukuru maafisa wa msafara wa hija wa Iran kwa kuendesha vizuri kazi hiyo na akasema kuwa licha ya kazi nzuri zilizofanyika lakini hatupasi kufumbia macho nakisi na kasoro zilizokuwepo. Ametilia mkazo suala la kupunguzwa kasoro hizo hadi kufikia kiwango cha kuridhisha.
Ayatullah Khamenei amesema watu wanaokwenda hija wanapatwa na mabadiliko makubwa kwa kushuhudia usafi, masuala ya kiroho na adhama ya maeneo matukufu ya Makka na Madina, lakini jambo muhimu zaidi ni kulinda matunda hayo ya kiroho.
707875



captcha