Baada ya kuwasili katika maonyesho hayo ya teknolojia ya kistratijia, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu alielekea moja kwa moja katika eneo lililotengwa makhsusi kwa ajili ya kuwakumbuka mashahidi Ali Muhammadi na Dakta Shahriyari na kuwasomea al Fatiha na dua mashahidi hao wa sayansi na maarifa.
Katika maonyesho hayo kunaonyehwa uvumbuzi wa wasomi na wataalamu wa Iran kwenye medani za teknolojia ya anga, teknolojia ya mikroelektroniki, nishati jadidika, nano teknolojia, teknolojia ya mawasiliano, teknolojia ya seli shina na elimu ya tiba. 763863