IQNA

Iran yaandaa maonyesho ya Qur'ani katika nchi 40

14:23 - August 03, 2011
Habari ID: 2164671
Mkuu wa Shirika la Iran la Utamaduni na Uhusiano wa Kiislamu ICRO amesema kuwa shirika hilo limeandaa maonyesho na vikao kadhaa vya Qur'ani na kidini katika zaidi ya nchi 40 katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.
"Ramadhani ni chimbuko la Qur'ani Tukufu na sisi katika ICRO tunajitahidi kuandaa programu mbalimbali za Kitabu Kitukufu kote duniani".
Dkt. Mohammad Bagher Khorramshad ameongeza kuwa, hivi karibuni, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliitaja Qur'ani kuwa nukta muhimu ya umoja, heshima na nguvu ya umma wa Kiislamu. 'Kwa hivyo katika mipango yetu tumezingatia kwa kina nafasi ya Qur'ani katika kuimarisha umoja wa Kiislamu'. Amesema 'Wiki ya Qur'ani' itafanyika katika nchi 20 za Asia, Afrika na Ulaya. Nchi hizo ni pamoja Sweden, Uingereza, Canada, Russia, Uturuki, Pakistan, Malaysia, Tunisia, Ufaransa na Kenya'.
836070
captcha