Kituo cha habari cha The Hindu kimeripoti kuwa utumiaji wa kalamu na simu hiyo ya mkononi unamuwezesha mtumiaji kusoma matini ya sura za Qur'ani, tarjumi ya kitabu hicho kwa lugha 19 tofauti na kusikiliza kiraa ya Qur'ani ya makarii na wasomaji 16 mashuhuri duniani.
Kalamu na simu hiyo ambavyo vimetengenezwa nchini Uchina vimeanza kuuzwa katika mji wa Bombay na miji mingine kadhaa ya India.
Simu na kalamu hiyo vinamuwezesha mmiliki kusoma tafsiri na tarjumi za Qur'ani kwa lugha kama Kiingereza, Kiurdu, Bengali, Malai, Tamil, Pashtu, Kifarsi, Dari, Kituruki, Kifaransa, Kijerumani, Kirussia na Kichina.
Mbali na hayo kalamu na simu hiyo pia vina vitabu 33 vya maudhui mbalimbali za Kiislamu, adhana, matangazo ya wakati wa kisheria wa swala, uwezo wa kuainisha upande wa kibla na kadhalika. 1046996