Amesema kuwa iwapo wanachama wa jumuiya hiyo zitakuwa na ushirikiano mkubwa katika fremu ya NAM, hapana shaka kwamba jitihada za madola ya kidhalimu za kuyawekea vikwazo na mashinikizo nchi zinazojitawala zitaambulia patupu.
Amesisitiza kuwa sharti la kuwepo ushirikiano mkubwa wa nchi wanachama wa NAM ni kuanzishwa taasisi madhubuti za utendaji na kuongeza kuwa, madola ya kibeberu yanaeneza propaganda kwamba haiwezekani kusimama kidete mbele yao, lakini wananchama wa jumuiya ya NAM wanaweza kuthibitisha kinyume cha madai hayo ya kipropaganda.
Katika mazungumzo hayo Rais Sheriff Namajo wa Guinea Bissau ameeleza hamu ya nchi yake ya kustawisha zaidi uhusiano na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyanja mbalimbali. 1089005