Ayatullahil Udhmaa Ali Khamenei ameyasema hayo Jumatatu mjini Tehran katika mazungumzo yake na Katibu Mkuu wa Harakati ya Wananchi ya Ukombozi wa Palestina, Ahmad Jibril. Amepongeza huduma na juhudi kubwa za Katibu Mkuu wa harakati hiyo katika njia ya kupigania malengo ya Wapalestina na akasema: Ahmad Jibril ni miongoni mwa nguzo muhimu za kadhia ya Palestina.
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameeleza matarajia kwamba mapambano ya Palestina yataendelea hadi utakapopatikana ushindi wa mwisho.
Kwa upande wake Ahmad Jibril ameeleza kufurahishwa kwake na kukutana na Kiongozi Muadhamu na kusema Mapinduzi ya Kiislamu yameifanya Iran kuwa nchi yenye taathira kubwa katika uwanja wa kimataifa na kwamba maendeleo ya sasa ya Iran yamepatikana chini ya usimamizi wa busara na hekima wa Walii wa Waislamu duniani Ayatullah Ali Khamenei. Ahmad Jibril pia amepongeza misimamo imara ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kutetea haki za taifa la Palestina.