IQNA

Amnesty yaitaka serikali ya Nigeria imuachilie huru Sheikh Zakzaky

21:54 - January 16, 2017
Habari ID: 3470799
IQNA-Shirika la kutetea haki za binadmau la Amanesty International limeitaka serikali ya Nigeria kumuachulia huru kiongozi wa Harakati ya Kiislamu, Sheikh Ibrahim Zakzaky.
Katika taarifa, Amnesty International imesema serikali ya Nigeria inapaswa kutekeleza amri ya Mahakama ya Juu ya Fiderali ambayo ilitoa muhula wa siku 45 kwa serikali kumuachilia huru Sheikh Zakzaky, muhula ambao umemelizika jana Jumapili.
Wakati huo huo, Ibrahim Mussa, Msemaji wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria ametoa taarifa maalumu ambapo mbali na kutahadharisha kuhusiana na kupuuzwa amri ya mahakama ya nchi hiyo kuhusiana na kuachiliwa huru Sheikh Zakzaky amesisitiza kuwa, njama za viongozi wa serikali ya Abuja za kuchafua sura ya Harakati ya Kiislamu ya Nigeria hazitazaa matunda.

Ibrahim Mussa ameeleza kuwa, nyaraka zilizofichuliwa na duru za kuaminika na ambazo ziko karibu na mashirika ya kijasusi ya nchi hiyo zinaonesha kuwa, baadhi ya mamluki wa ndani na wa nje wanafanya njama za kukiuka amri ya mahakama inayotaka kuachiliwa huru Sheikh Zakzaky.

Kwingineko, Sheikh Ibrahim Zakzaky ambaye anashikiliwa katika jela ya Nigeria ametoa ujumbe akisema hana wasiwasi kuhusu kuendelea kushikiliwa jela au kuachiwa huru, kwa sababu Mwenyezi Mungu Muweza huwatunuku kheri waja wake popote pale walipo.

Ripoti zinasema kuwa serikali ya Nigeria haijachukua hatua yoyote ya kumwachia huru au kubadilisha mwenendo wake kuhusu Sheikh Ibrahim Zakzaky na kwamba jeshi la Nigeria linakwamisha uamuzi huo.
Mapema mwezi Disemba mwaka uliopita Jaji Gabriel Kolawole wa Mahakama Kuu ya Nigeria aliiamuru serikali na Nigeria kumwachilia huru bila ya masharti yoyote Sheikh Zakzaky na mke wake katika kipindi cha siku 45 zijazo.   

Sheikh Ibrahim Zakzaky akiwa na mke wake alitiwa mbaroni na Jeshi la Nigeria mwezi Disemba mwaka 2015 katika kituo  cha kidini huko katika mji wa Zaria kaskazini mwa jimbo la Kaduna. Tokea wakati huo Sheikh Zakzaky na mkewe wamekuwa wakizuiliwa katika mojawapo ya vituo vya kijeshi vya nchi hiyo bila kufunguliwa mashktaka.

Jeshi hilo lilidai kuwa wafuasi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria walikuwa na njama ya kutaka kumuua Mkuu wa Jeshi la Nigeria, madai ambayo yamekanushwa vikali na wafuasi wa harakati hiyo.

Jeshi hilo katili liliizika miili ya waliouawa katika kaburi moja kwa lengo la kuficha ushahidi wa ukubwa wa jinai hiyo. Inakadiriwa kuwa Waislamu 1000 wasio na hatia waliuawa katika tukio hilo huku Sheikh Zakzaky, ambaye hali yake ya kiafya si nzuri, akiendelea kushikiliwa korokoroni pasina kufunguliwa mashtaka.

3563307



captcha