IQNA

Madagascar yafunga Madrassah 16 za Qur'ani

19:59 - May 05, 2017
Habari ID: 3470969
TEHRAN (IQNA)-Serikali ya Madagascar imetangaza uamuzi wa kufunga madrassah na taasisi 16 za kufunza Qur'ani nchini humo hatua ambayo imewakasirisha Waislamu nchini humo.
Taarifa zinasema Wizara ya Elimu ya Madagascar imetumia kisingizio cha kukosekana suhula za kutosha kuwa sababu ya kufunga madrassa hizo za Qur'ani. Waziri wa Elimu katika nchi hiyo amezungumza kupitia radio ya taifa na kudai kuwa: "Taasisi hizi 16 awali zilianzisha kama madrassah binafsi za Kiislamu lakini hivi sasa zimegeuzwa na kuwa vituo vya kutoa mafunzo kamili na ya umma ya Qur'ani."
Amesema yuko tayari kukutana na wawakilishi wa Waislamu nchini humo ili kutoa ufafanuzi kuhusu uamuzi wake na kuongeza kuwa, uamuzi huo utaanza kutekelezwa baada ya kumalizika muhula huu wa masomo.
Uislamu umekuwepo nchini Madagascar  hata kabla ya Ukristo kuanzia karne za 10 na 11 Miladia ambapo Waislamu wanakadiriwa kuwa takribani asilimia 10 ya watu wote milioni 24 katika nchi hiyo ambayo ni kisiwa kikubwa katika pwani ya kusini mashariki mwa Afrika. Uislamu uliingia Madagascar kupitia wahajiri kutoka nchi za bara Arabu na Zanzibar.

3596267
captcha