IQNA

Hali mbaya ya Waislamu wa madhehebu ya Shia, Awamiyah Saudi Arabia

18:27 - May 19, 2017
Habari ID: 3470985
TEHRAN (IQNA)- Wanajeshi wa Saudi Arabia wanaendelea kuwaua na kuwakandamiza Waislamu wa madhehebu ya Shia katika mji wa al-Awamiyah mashariki mwa nchi hiyo.
Hali mbaya ya Waislamu wa madhehebu ya Shia, Awamiyah  Saudi Arabia

Duru za kuaminika zinadokeza kuwa watu kadhaa wameuawa shahidi hadi sasa tokea utawala wa Saudi Arabia uanzisha mzingrio dhidi ya mtaa wa Al-Mosara katika mji wa Awamiyah.

Ikiwa ni katika kushadidisha hujuma zao za kijeshikatika kitongoji cha al-Awamiyah,vikosi vya usalama vya Aal Saud vimechukua hatua zenye lengo la kuwazingira Waislamu wa madhehebu ya Shia wa eneo hilo huku vikitumia mabomu na risasi zinazozalisha moto kwa ajili ya kuchoma nyumba za eneo hilo. Katika siku za hivi karibuni kufuatia kushadidi hujuma na mashambulio ya utawala wa Aal Saud katika maeneo ambayo ni ya Mashia mashariki mwa nchi hiyo, mamia ya Waislamu hao wa Kishia wameuawa.

Kuendelea mauaji dhidi ya Waislamu wa Kishia yanayofanywa na utawala wa Aal Saud kumezifanya jinai za familia hiyo zizidi kuonekana. Utawala wa familia yaAal Saud nchini Saudia badala ya kuchukua hatua zitakazopelekea kupunguza malalamiko na upinzani dhidi yake kwa kuwaridhisha wananchi, umeamua kutumia mkono wa chuma dhidi ya mrengo wa upinzani.

Katika miaka ya hivi karibuni utiaji mbaroni kiholela, mateso, ukandamizaji na kutolewa hukumu zisizo za kiadilifu ni mambo ambayo yameshuhudiwa yakiongezeka mno nchini Saudia, ambapo mauaji dhidi ya Mashia ni kilele cha ukatili wa utawala huo.

Kushadidi ukandamizaji dhidi ya Waislamu wa Kishia si tu kwamba, hakujawa na faida yoyote kwa utawala wa Riyadhbali kumeufanya mgogoro wa ndani nchini humo uzidi kutokota na kushika kasi. Baada ya Saudia kushadidisha vitendo vya ukandamizaji katika maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo ambapo akthari ya wakazi wake ni Waislamu wa madhehebu ya Shia, kumeibuka malalamiko makubwa katika maeneo hayo na kupelekea kuzuka makabiliano baina ya vikosi vya usalama na raia wa kawaida.

3600954

captcha