IQNA

Algeria kurekebisha mfumo wa usomeshaji Qur'ani shuleni

7:52 - May 23, 2017
Habari ID: 3470991
TEHRAN (IQNA)-Algeria imetangaza mpango wa kurekebisha mfumo wa usomeshaji Qur'ani katika shule za nchi hiyo kwa ushirikiano na wadau wa masuala ya kidini nchini humo.

Ridhwan Ma'ash Al-Jumuah, Katibu Mkuu wa Wizara ya Masuala ya Dini na Waqfu katika jimbo Ghardaia ameyasema hayo katika mkutano wa pili wa kitaifa wa Usomeshaji Qur'ani Tukufu ambao umefanyika kwa kaulimbiu ya "Mbinu za Usomeshaji Qur'ani; Malengo na Nyenzo".

Ma'ash Al-Jumua'h amebainisha kuwa hatua hiyo inachukuliwa kwa lengo la kuimarisha umoja wa kidini kwa ushirikiano wa wadau na wanaharakati wa masuala ya kidini.

Inafaa kuashiria hapa kuwa mkutano wa pili wa kitaifa wa Usomeshaji Qur'ani Tukufu umefanyika katika jimbo la Ghardaia lililoko kusini mwa Algeria kwa kuhudhuriwa na Mashekhe, Maimamu wa Sala ya Ijumaa na Wanaakademia wa Vyuo Vikuu kwa madhumuni ya kubuni mbinu na utaratibu wa aina moja wa usomeshaji Qur'ani Tukufu.

Washiriki wa mkutano huo wamehudhuria mafunzo ya amali na kubadilishana mawazo juu ya mustakabali wa usomeshaji Qur'ani na mbinu za kujadidisha usomeshaji huo kwa kufuata misingi ya kadiri na wastani.

3601638

captcha