Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, Husseini ametangazwa mshindi katika mashindano hayo yaliyoanza Ijumaa mjini Istanbul katika Msikiti wa Fatih.
Kulikuwa na washiriki 120 kutoka nchi 62 katika vitengo vya kusoma na kuhifadhi Qur'ani Tukufu. Baada ya awamu ya kwanza quraa 10 walifika katika fainali akiwemo Sayyed Mostafa Husseini wa Iran paoja na wawakilishi Tunisia, Philippines, Indonesia, Bangladesh, Yemen, Uturuki, Malaysia, Brunei, na Pakistan.
Washindi katika kitengo cha kuhifadhi Qur'ani watatangazwa baadaye. Mashindnao hayo ya Qur'ani huandaliwa kila mwaka na Idara ya Masuala ya Kidini (Diyanet) katika ofisi ya rais wa Uturuki.