TEHRAN (IQNA)-Waislamu wa eneo la Qatif nchini Saudi Arabia wanaombolezo mauji ya kidhalimu mwalimu wa Qur'ani Tukufu, Amin al Hani, aliyepigwa risasi na kuuwa shahidi na wanajeshi wa utawala wa kiimla wa Saudi Arabia.
Kwa mujibu wa mwandishi wa
IQNA, katika hali ambayo Jumamosi 24 Juni wiki iliyopita Waislamu kote duniani
waikuwa wakikaribia kumaliza Saumu ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani huku
wakijitayarishwa kwa ajili ya Siku Kuu ya Idul Fitr, Waislamu wa Saudia hasa
Waislamu wa madhehebu ya Shia eneo la Qatif walishuhudia jinai ya wanajeshi wa
utawala wa Saudi Arabia ambao walimuua shahidi kidhalimu mwalimu na
mwanaharakati wa Qur'ani Tukufu Amin al Hani.
Tukio hilo lilijiri Jumamosi
usiku wakati wanajeshi walipofyatulia risasi gari la Amin al Hani akiwa
analiendesha katika mji wa Awamiyah ulio eneo la Qatif lenye wakaazi wengi
Waislamu wa madhehebu ya Shia. Baada ya gari hilo kufyatuliwa risasi
liliteketea moto na baadaye mwili wa marehemu al Hani ulipatikana ndani ya gari
hilo. Ilibidi wataalamu watumie mbinu ya kupima vinasaba (DNA) ili kuutambua
mwili wa Shahidi Hani, haukuweza kutambulika kutokana na moto mkali
uliomteketeza.
Video ya tukio hilo imeenea
katika mitandao ya kijamii na kuibua hasira ya wakaazi wa eneo hilo.
Shahidi Hani alikuwa pia
mwenyekiti wa baraza la Qur'ani katika mji Awamiya katika eneo la Qatif na
wanajeshi katili wa ufalme wa Saudia walimuua shahidi akiwa anarejea kutoka
katika majlisi ya Qur'ani Tukufu.
Maulamaa wa Kishia nchini
Saudi Arabia wamebainisha masikitiko yao makubwa kufuatia kuuawa shahidi Ustadh
Hani na kusema ameacha pengo kubwa sana katika jamii ya watu wa Qatif na Saudi
Arabia kwa ujumla. Kutokana na nafasi yake katika harakati za Qur'ani, Hani
ametajwa kuwa Shahidi wa Qur'ani. Mauaji ya msomi huyo wa Qur'ani Tukufu ni
sehemu nyingine ya jinai zisizo na kikomo za ukoo wa Aal Saud ambao unakali
ardhi ya Hijaz iliyopachikwa jina la Saudi Arabia.