Sheikh Gomaa amebainisha kuwa wanafunzi katika shule hizo hawatatozwa karo na kwamba wanaofunza katika shule hizo wanapaswa kuwa wamehifadhi Qur’ani Tukufu kikamilifu na wasiwe na misimamo mikali ya kidini.
Misri ni nchi iliyo kaskazini mwa Afrika na ina idadi ya watu karibu milioni 95 ambapo Waislamu ni asilimia 90 ya watu wote nchini humo. Harakati Za Qur’ani nchini Misri zina historia ndefu inayonawiri na nchi hiyo inaongoza kwa quraa au wasomaji bora wa Qur’ani duniani.