Katika mpango huo wa kuwahimiza watoto kuswali Sala ya Jamaa, wametunukiwa zawadi za baiskeli katika Msikiti wa Sultan Selim katika mtaa wa Fatih mjini Istanbul.
Wazazi wengi wamekuwa wakienda na watoto wao msikitini ili kuwahimiza kuendeleza amali hiyo njema ya kusali Sala ya Alfajiri katika jamaa.
Uwanja wa msikiti wiki hii ulikuwa umejaa baiskeli huku kukiwa na furaha miongoni mwa watoto walipopokea zawadi hizo.
Inatazamiwa kuwa ubunifu huo utaimarisha imani ya watoto ili waweze kuenda msikitini wakati wa Sala ya Alfajiri.
3651924