IQNA

Mzee mwenye umri wa miaka 65 ahifadhi Qur'ani kwa muda wa miezi 10

20:00 - November 03, 2017
Habari ID: 3471246
TEHRAN (IQNA)-Mzee mwenye umri wa miaka 65 mjini Jeddah, Saudi Arabia, amefanikiwa kuhifadhi Qur'ani Tukufu kikamlifu kwa muda wa miezi 10.

Mzee mwenye umri wa miaka 65 ahifadhi Qur'ani kwa muda wa miezi 10Abdullah al-Jurjawi ametajwa kuwa mtu mwenye umri wa juu zaidi kufanikiwa kuhifadhi Qur'ani Tukufu mjini Jeddah katika mwaka 1438 Hijria Qamaria (2016/2017).

Katika mahojiano na gazeti la Okaz la Saudia, amesema tokea zama za ujana wake alikuwa anasoma kurasa mbili za Qur'ani kila siku lakini alianza kuhifadhi Qur'ani Tukufu baada ya kustaafu mwaka jana.

"Punde baada ya kustaafu, nilimfuata Ustadh Majid Bijash katika Msikiti wa Ahl al-Khair, na Alhamdulillah, nilifanikiwa kuhifadhi Qur'ani kwa muda wa miezi 10."

Tayari al-Jurjawi ameshafanya mtihani wa kuhifadhi Qur'ani Tukufu katika Jumuiya ya Qur'ani ya Khayrukum mjini Jeddah.Mzee mwenye umri wa miaka 65 ahifadhi Qur'ani kwa muda wa miezi 10

Jumuiya hiyo imesema itamuenzi kikamilifu al-Jurjawi katika hafla maalumu siku za usoni.

3464319

captcha