Kufuatia uamuzi huo, Katibu Mkuu wa Baraza la Waislamu Uingereza, Harun Khan amebainisha wasi wasi wake kwamba Ofsted imetangaza kuwalenga na kuwasaili wasichana wa shule wanovaa mtandio.
"Ujumbe wa wazi hapa kwa wanawake wote Uingereza wanaovaa hijabu ni kuwa wao ni raia wa daraja ya pili, "amesema Khan.
Aidha amebainisha masikitiko yake kuwa hivi sasa kubaguliwa wanaovaa hijabu ni sera nchini Uingereza. Amesema sera kama hivyo itakuwa na matokeo ambayo hayakukusudiwa huku akisisitiza kuwa wazazi Waislamu na watoto wao wana haki ya maamuzi na hawapaswi kupuuzwa
Waislamu ni takriabni asilimia 4.4 ya watu wote Uingereza na ni jamii ya waliowachache inayostawi kwa kasi zaidi.