IQNA

Washindi wa Mashindano ya Qur'ani ya Wanachuo wa Vyuo vya Kidini Wazawadiwa

17:53 - April 25, 2018
Habari ID: 3471480
TEHRAN (IQNA) – Washindi wa Mashindano ya pili ya Kimataifa ya Qur'ani ya wanafunzi wa vyuo vya kidini (Hawza) wametangazwa katika sherehe iliyofanyika Jumapili.

Kwa mujibu wa jopo la majaji, Mohammad Zahedi alishika nafasi ya kwanza katika kategoria ya qiraa ya Qur'ani na ufahamu ya misingi ya Qur'ani.

Ali Hassan Abdul Aa’la wa Iraq na Mohammad Reza Nouri wa Afghanistan waliibuka wa pili na wa tatu kwa taratibu.

Katika kategoria ya kuhifadhi Qur'ani Tukufu kikamilifu na ufahamu wa misingi ya Qur'ani, mwakilishi wa Iran Mahamoud Norouzi alishika nafasi ya kwanza. Nafasi ya pili imechukuliwa na Ahmad Yasri wa Misri huku Mohammad Tijani wa Ghana akishika nafasi ya tatu.

Sherehe za kufunga mashindano hayo zilihudhuriwa na wanazuoni wa ngazi za juu wakiwemo  mwanazuoni mtajika Ayatullah  Jafar Sobhani, mkurugenzi wa vyuo vya kidini vya Kiislamu nchini Iran, Ayatullah Ali Reza Aarafi, and na mkuu wa Shirika la Wakfu, Hujjatul Islam Ali Mohammadi.

Mashindano ya mwaka huu yaliyoafunguliwa rasmi Jumatano iliyopita yanjumuisha Mashindano ya 35 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran (ya kawaida maalumu kwa ajili ya wanaume) na pia kunafanyika mashindano mengine ya Qur'ani ya wanawake, ya wenye ulemavu wa macho, ya wanafunzi wa vyuo vikuu na ya wanachuo wa vyuo vya kidini.

Mashindano hayo ya kimataifa ya Qur'ani yanayofanyika kwa kaulimbiu ya "Kitabu Kimoja, Umma Mmoja" sambamba na kuanza sherehe za mwezi huu mtukufu wa Shaaban yanawajumuisha wasomaji (quraa)   na waliohifadhi (hufadh)  Qur'ani  258 kutoka nchi 84.

/3708866

captcha