Sheikh al Tayyib amelaani pia vitendo vya magenge ya kigaidi vya kujichukulia sheria mikononi mwao na kutenda jinai mbaya kwa jina la Uislamu na kusisitiza kuwa, magenge hayo ya kigaidi hayana uhusiano wowote na dini tukufu ya Kiislamu.
Amesema hayo wakati alipoonana na wakurugenzi wa vyombo zaidi ya 40 vya habari pamoja na wahariri kutoka nchi 23 za Afrika ambao walimtembelea katika Chuo Kikuu cha al Azhar, mjini Cairo, Misri.
Amesema, dini tukufu ya Kiislamu, ni dini ya amani na kupendana, na inapinga vikali jinai za kukata watu vichwa na utegaji mabomu unaofanywa na magenge ya kigaidi kwa lengo la kuharibu sura ya dini ya Kiislamu.
Wakurugenzi wa zaidi ya vyombo 40 vya habari na wahariri kutoka zaidi ya nchi 23 za Afrika, hivi sasa wako Cairo, mji mkuu wa Misri kwa ajili ya mafunzo ya mwezi mmoja kuhusiana na vyombo vya habari barani Afrika.
Chuo Kikuu cha al Azhar ni moja ya vyuo vikuu vikongwe katika ulimwengu wa Kiislamu na vimekuwa vikipokea wanafunzi kutoka kona zote za dunia.
3499996