IQNA

Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu:

Suna ya wakfu ienezwe zaidi katika jamii

19:10 - March 13, 2012
Habari ID: 2291287
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei adhuhuri ya leo Jumanne amekutana na wafanyakazi wa Jumuiya ya Wakfu na Masuala ya Kheri ya Iran na kusisitiza kuwa wakfu ni taasisi bora ya kidini na kwamba kuna udharura wa kuenezwa zaidi suna hiyo ya kutoa wakfu katika jamii kwa kuwahamasisha watu kufanya amali hiyo na kutekeleza kwa njia sahihi haki za watu wanaotoa wakfu.
Amesema kuwa jambo muhimu zaidi katika wakfu ni kuchunga amana katika suala hilo.
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa maudhui ya wakfu ni pana mno na kuongeza kuwa, kwa sasa kuna nyanja nyingi kwa ajili ya wakfu ikiwa ni pamoja na medani za tiba, elimu, uhakiki na utafiti, sayansi za kisasa, mazingira na kueneza dini kwa njia za kisasa.
Ayatullah Ali Khamenei amesisitiza juu ya umuhimu na udharura wa viongozi na wakurugenzi kusimamia vyema taasisi za wakfu na kusema kuwa usimamizi huo una maana ya kutekeleza majukumu kwa njia sahihi na kamili katika maudhui muhimu sana ya wakfu.
Amepongeza na kushukuru pia juhudi kubwa zilizofanywa na Hujjatul Islam Walmuslimin Muhammadi ambaye ni Mkuu wa Jumuiya ya Wakfu na Masuala ya Kheri hapa nchini, wakurugenzi na wafanyakazi wa taasisi hiyo. 971492

captcha