IQNA

Uchunguzi wa Maoni

Waislamu wengi Uingereza wanaamini hujuma za 9/11 ni njama ya Marekani, Mayahudi

0:29 - December 04, 2016
Habari ID: 3470715
IQNA: Uchunguzi wa maoni umebaini kuwa Waislamu wengi Uingereza wanaamini kuwa serikali ya Marekani ndiyo iliyotekeleza hujuma za kigaidi nchini humo Septemba 11, 2001.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa maoni, asilimia 31 ya Waislamu Uingereza wanaamini kuwa serikali ya Marekani ilihusika moja kwa moja katika hujuma zilizotekelezwa dhidi ya majengo pacha ya Kituo cha Biashara Duniani mjini New York na dhidi ya jengo la Pentagon mjini Washington. Uchunguzi huo wa taasisi ya Policy Exchange umebaini kuwa ni asilimia nne tu ya Waislamu Uingereza wanaoamini taarifa rasmi kuwa kundi la Al Qaeda ndilo lililotekekeza hujuma hiyo ya kigaidi ya Septemba 11, 2001.

Halikadhalika asilimia 7 ya Waislamu Uingereza wanaamini kuwa hujuma hizo za kigaidia zilitekelezwa na Wazayuni (Mayahudi) na wala si Al Qaeda. Uchunguzi huo uliowahusisha Waislamu 3,000 unaoneysha kuwa asilimia 52 wanasema hadi sasa hawawezi kubaini kwa hakika ni nani aliyetekeleza hujuma hiyo ya kigaidi. Itakumbukwa kuwa baada ya hujuma za 9/11 kulishuhudiwa wimbi kubwa la chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu katika nchi za Magharibi.

Kwingineko, uchunguzi huo wa maoni umebaini kuwa asilimia 71 ya Waingereza wasiokuwa Waislamu wanaamini kundi la Al Qaeda ndilo lililotekeleza hujuma hiyo huku asilimia 10 wakiamini ni Rais wa wakati huo wa Marekani, George W Bush ndie aliyetekeleza hujuma hiyo na wengine asilimia moja wakisema ugaidi huo ulitekelezwa na Wazayuni.

Waislamu wengi Uingereza wanaamini hujuma za 9/11 ni njama ya Marekani, Mayahudi

Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2011, idadi ya Waislamu Uingereza ni takribani Milioni tatu au asilimia 5 ya wakaazi wa nchi hiyo ya Ulaya Magharibi.

3550513
captcha