Ishirini na tatu kati yao walikuwa ni wanawake ambao wamehifadhi Qur'ani Tukufu kikamilifu kwa kuhudhuria kozi zilizoandaliwa na vituo vya Dar al-Salam, Othman bin Affan na Nur al-Quran.
Idadi kubwa ya wananchi pamoja na maafisa wakuu wa serikali na wanadiplomasia wa kigeni walihudhuria hafla hiyo.
Guinea ni nchi iliyoko Afrika Magharibi, inayopakana na Bahari ya Atlantiki upande wa magharibi.
Takriban asilimia 85 ya wakazi wa Guinea ni Waislamu, hasa wa madhehebu za Sunni. Waislamu ni wengi katika maeneo yote manne ya kijiografia. Wakristo, wengi wao wakiwa Wakatoliki, wanajumuisha asilimia 8 ya walio wachache.
Qur'ani Tukufu ndio Maandiko pekee ya kidini ambayo yanahifadhiwa kikamilifu moyoni wafuasi wake.
Watu wasiohesabika katika kila umma wa Kiislamu wamehifadhi Qur'an tangu siku ya kwanza ilipoteremshwa.
Qur'ani Tukufu ina Juzuu 30, Sura 114 na aya 6,236.
4114969