IQNA

Harakati za Qur'ani Afrika

Waliohifadhi Qur'ani Tukufu nchini Guinea waenziwa

19:21 - January 16, 2023
Habari ID: 3476414
TEHRAN (IQNA)- Jumla ya watu 190 ambao wamejifunza Qur'an Tukufu kikamilifu kwa moyo walitunukiwa zawadi na kuenziwa katika sherehe hiyo iliyofanyika katika Uwanja wa Jenerali Lansana Conté.

Ishirini na tatu kati yao walikuwa ni wanawake ambao wamehifadhi  Qur'ani Tukufu kikamilifu kwa kuhudhuria kozi zilizoandaliwa na vituo vya Dar al-Salam, Othman bin Affan na Nur al-Quran.

Idadi kubwa ya wananchi pamoja na maafisa wakuu wa serikali na wanadiplomasia wa kigeni walihudhuria hafla hiyo.

Guinea ni nchi iliyoko Afrika Magharibi, inayopakana na Bahari ya Atlantiki upande wa magharibi.

Takriban asilimia 85 ya wakazi wa Guinea ni Waislamu, hasa wa madhehebu za Sunni. Waislamu ni wengi katika maeneo yote manne ya kijiografia. Wakristo, wengi wao wakiwa Wakatoliki, wanajumuisha asilimia 8 ya walio wachache.

Qur'ani Tukufu ndio Maandiko pekee ya kidini ambayo yanahifadhiwa kikamilifu moyoni wafuasi wake.

Watu wasiohesabika katika kila umma wa Kiislamu wamehifadhi Qur'an tangu siku ya kwanza ilipoteremshwa.

Qur'ani Tukufu ina Juzuu 30, Sura 114 na aya 6,236.

Quran Memorizers Honored in Guinea

Quran Memorizers Honored in Guinea

Quran Memorizers Honored in Guinea

 

4114969

 

captcha