Tarehe ya leo inasadifiana pia na kumbukumbu za siku ya kuzaliwa Imam Jafar Sadiq AS.
Mkutano wa 29 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu ambao umeshirikisha wanazuoni, wanafikra na wasomi kutoka nchi 70 duniani unatazamiwa kufunga pazia lake hii leo hapa mjini Tehran.
Siku kama ya leo yaani tarehe 17, mwezi wa Mfunguo Sita (Rabiul Awwal),
miaka 1490 iliyopita kwa mujibu wa nukuu za maulama wengi wa Kiislamu,
alizaliwa Mtume Muhammad SAW katika mji mtakatifu wa Makka. Hata hivyo
baadhi ya wapokezi wa Historia wanaitakidi kuwa, Mtume huyo Uislamu
alizaliwa tarehe 12 Rabiul Awwal.
Mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Imam Khomeini MA alitangaza
kipindi cha baina ya tarehe 12 na 17 Mfunguo Sita kuwa Wiki ya Umoja wa
Kiislamu, kwa lengo la kuwaleta pamoja Waislamu pasi na kujali madhehebu
yao, ili kwa pamoja wayatafutie ufumbuzi matatizo yanayoukabili
ulimwengu wa Kiislamu.
Idhaa ya Kiswahili Sauti ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inatoa mkono wa kheri na fanaka kwa Waislamu na wapenda haki kote duniani kwa mnasaba wa siku hii adhimu, ya kukumbuka kuzaliwa Mtume wa mwisho Muhammad al Mustafa SAW.