IQNA

Azhar yalaani hujuma dhidi ya misikiti ya Diyala, Iraq

15:33 - January 14, 2016
Habari ID: 3470042
Chuo Kikuu cha al-Azhar nchini Misri kimelaani vikali mashambulizi ya kigaidi dhidi misikiti saba katika mji wa al-Miqdadiyah, katika mkoa wa Diyala nchini Iraq.
Kwa mujibu wa tovuti ya egynews.net, taarifa iliyotolewa Alhamisi  na chuo hicho imelaani vikali mashambulizi hayo yaliyofanywa na watu wenye silaha ambao baada ya kutekeleza hujuma hizo walitoa vitisho dhidi ya Waislamu wa eneo hilo kuhakikisha wanahama mara moja eneo hilo na kwamba watauawa endapo hawatofanya hivyo. Taarifa hiyo mbali na kukitaja kitendo hicho kama uovu wa kuchupa mipaka, pia imekitaja kuwa si cha ubinaadamu. Aidha taarifa hiyo ya al-Azhar imesisitiza kuwa, dini Tukufu ya Uislamu inayovitambua vitendo hivyo vilivyo kinyume na mafundisho ya dini hiyo na utu na ubinaadamu, inavitaja kuwa ni kosa ambalo ni haramu kabisa. Imeyataka makundi ya wabeba silaha kuheshimu matukufu ya kidini hususan nyumba za Mwenyezi Mungu kama ambavyo imewataka Waislamu wa Iraq kujiepusha na kila aina ya uchochezi wa kidini au njama zozote zenye lengo la kuigawa nchi hiyo.

Itakumbuwa kuwa siku ya Jumanne watu wenye silaha walishambulia kwa mabomu ya moto misikiti saba na mamia ya maduka ya mji huo wa al-Miqdadiyah na kuwaua watu wasiopungua 24. Magaidi wakufurishaji wa kundi la ISIS au Daesh wamejigamba kuhusika na hujuma dhidi ya misikiti hiyo.

3467292


captcha