IQNA

Bikizee asiyejua kusoma ahifadhi Qur'ani Imarati

0:15 - January 26, 2016
1
Habari ID: 3470090
Bikizee mwenye umri wa miaka 82 asiyejua kusoma amefanikiwa kuhifadhi juzuu 10 za Qur'ani Tukufu.
Kwa mujibu wa tovuti ya KTimes, Sheikha Dhaan Saeed Al Suraidi mwenye umri wa takribani miaka 82 kutoka kitongoji cha  Adhan huko Ras al Kheima, Umoja wa Falme za Kiarabu au Imarati, amehifadhi juzuu hizo za Qur'ani Tukufu na umri wake haukuwa kizingiti.
Aidha pamoja na kuwa hajui kusoma wala kuandika, kwa kutegemea irada yake iamra ameweza kujifunza  Qur'ani Tukufu.
Yeye ni ajuza mwenye ustadi na ambaye anajishughulisha na ukulima wa kifugo na pia ni mtaalamu wa tiba ya miti shamba.
Ummu Muhammad ameweza kuhifadhi Qur'ani kwa urahisi kwa kutumia vifaa vya kidijitali vya kujifunza Qurani.
Akifafanua kuhusu namna alivyohifadhi Qur'ani anasema: "Misi siwezi kusoma wala kuandika lakini chombo hiki cha kidijitali ambayo kina uwezo wa kusoma aya za Qur'ani na kuzikariri nitakavyo kimenisaidia sana na hivyo nimeweza kuhifadhi Qur'ani kwa njia sahali."
Bikizee huyo aidha amejisajili katika kituo cha masomo ya Qur'ani katika eneo la Adhan ili aweze kuhifadhi juzuu zaidi za Qur'ani. Halikadhalika ametangaza nia yake ya kushiriki katika mashidano ya Qur'ani Imarati.
3470083
Imechapishwa: 1
Inatathminiwa: 0
Haiwezi kuchapishwa: 0
fesal khamis sultan
0
0
tushirikiane kusoma qur an kwa nguvu moja na kumuomba mungu atupe wepesi wa kuisoma qur ani tukufu kwa moyo mkunjufu
captcha