IQNA

Wabahrain waendeleza mwamko wa kupinga utawala wa kifalme

18:35 - May 01, 2016
Habari ID: 3470281
Watu wa Bahrain wamefanya maandamano wakitangaza mfungamano wao na wafungwa wengine wa kisiasa nchini humo.
Waandamanaji wametangaza mfungamano wao na wafungwa wa kisiasa akiwemo  Sheikh Ali Salman Katibu Mkuu wa Harakati ya Kiislamu ya Al-Wifaaq.Kadhalika katika maandamano hayo Wabahrain wamesisitizia umuhimu wa kufanyiwa marekebisho mfumo wa utawala nchini. Wakati huo huo wanaharakati wametangaza kuachiliwa huru Mahdi al-Musawi, mmoja wa viongozi wa Harakati ya Kiislamu ya al-Amal, baada ya kupitisha kipindi cha miaka mitano katika jela za utawala wa Aal-Khalifa. Al-Musawi akiwa na baadhi ya viongozi wa harakati ya al-Amali, akiwemo pia Muhammad Ali al-Mahfudh walihukumiwa na mahakama ya nchi hiyo kutumikia kifungo jela. Hii ni katika hali ambayo wafungwa wa kisiasa nchini Bahrain wamefanya mgomo wa chakula kulalamikia miamala mibaya ya utawala wa Aal-Khalifa dhidi yao. Katika fremu hiyo wafungwa wa jela ya al-Howdh al-Jaf wameanzisha mgomo wa chakula usio na kikomo. Inasemekana kwamba wafungwa nchini humo, wamekuwa wakiadhibiwa kwa kupigwa na kutukanwa. Kabla ya hapo pia, idara ya kupigania uhuru na shirika la kutetea haki za binaadamu zilizo chini ya harakati ya Kiislamu ya Al-Wifaaq zilitangaza kuwa, jumla ya watu 798 wanaendelea kushikiliwa katika korokoro za polisi na vituo vya uchunguzi wa makosa ya jinai, ambapo wamekuwa wakiteswa kwa kupewa adhabu mbalimbali. Mwaka jana viongozi wa Bahrain walitangaza kuwa, kwa akali watu 1765 walitiwa mbaroni ambapo 120 kati yao walikuwa ni watoto na 22 wakiwa ni wanawake. Aidha viongozi wa utawala huo wa Aal-Khalifa waliongeza kuwa, watu wengine 829 walikuwa wakizuiliwa katika majumba yao. Itafahamika kuwa, Bahrain imekuwa ikishuhudia maandamano ya amani ya wananchi tokea mwezi Februari mwaka 2011, ambapo utawala wa kidikteta wa nchi hiyo umekuwa ukishirikiana na askari wa Aal-Saud kuyakandamiza maandamano hayo. Katika mazingira hayo wanaharakati wa Bahrain kwa kuzingatia kuendelea maandamano hayo ya wananchi dhidi ya utawala wanasema kuwa, hivi sasa Aal-Khalifa wamefika kwenye mkwamo. Licha ya utawala wa Aal-Khalifa na Aal-Saud kutumia askari wa kigeni katika kukandamiza harakati ya wananchi, lakini bado wameshindwa kumaliza maandamano hayo na badala yake Wabahrain wamezidi kuwa na irada thabiti ya kuendeleza mwamko wa Kiislamu katika nchi hiyo ndogo ya Ghuba ya Uajemi.
3459682

captcha