IQNA

Hafidh wa Kenya apongeza kujitokeza wananchi wa Iran katika mashindano ya Qur'ani

15:38 - May 18, 2016
2
Habari ID: 3470318
Hafidh wa Qur'ani Tukufu kutoka Kenya aliyeshiriki Mashindano ya 33 ya Kimataifa ya Qur'ani ya Iran amepongeza kujitokeza kwa wingi wananchi wapendao Qur'ani wa Iran katika ukimbu wa mshindano.

Abdullah Yusuf Ismail mwakilishi wa wa Kenya na ambaye alifika katika fainali ya mashindano hayo amefanya mahojiano maalumu na mwandishi wa IQNA na kusema: "Ni mara ya kwanza nashiriki mashindano ya Qur'ani nchini Iran, na nina furaha kuweza kufika katika fainali ya mashindano haya."

Kuhusiana na jopo la majaji katika mashindano hayo amesema: "Kwa mtazamo wangu, jopo la majaji limefanya jitihada na kutoa maamuzi ya uadilifu."

Hafidh huyo wa Qur'ani kutoka Kenya amesema kuhudhuria kwa wingi wananchi Wairani katika ukumbi wa mashindano ya Qur'ani ni jambo ambalo limempa motisha katika kuweza kufanikiwa kufika fainali.

Abdullah Yusuf Ismail amesema amewahi kushiriki katika mashindano ya Qur'ani nchini Misri ambapo alishika nafasi ya pili katika kategoria ya kuhifadhi Qur'ani kikamilifu. Halikahdlika amesema kiwango cha mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Iran ni kizuri sana.

Aidha anasema amewahi kushiriki katika mashindano mengi ya Qur'ani nchini Kenya na kushika nafasi ya kwanza na kwa msingi huo aliteuliwa kuwa mwakilishi wa nchi hiyo katika Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Iran mwaka huu.

Mashindano ya 33 ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yalizinduliwa rasmi Jumatano iliyopita na kumalizika jana Jumanne katika Ukumbi Mkubwa wa Sala wa Imam Khomeini MA mjini Tehran.

Nchi zaidi ya 70 zilituma wawakilishi katika Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ambayo yalikuwa na washiriki 130. Kaulimbiu ya mashindano ya mwaka huu ilikuwa ni "Kitabu Kimoja Umma Moja”.

3498987

Imechapishwa: 2
Inatathminiwa: 0
Haiwezi kuchapishwa: 0
mwinyi ramadhani
0
0
Kwanza na wapongeza waandalizi wa mashindano haya ya kila mwaka , nikiwa mmoja niliechangia Hafidh Abdallah Yusuf , kuhudhuria mashindano hayo kama mfanya kazi wa kitengo cha utamaduni wa ubalozi wa Iran , Kenya , ni nani Imani kwamba huyu kijana akipewa nafasi mwakani atakuwa ni mwenye kupata namba za juu . Hata hivyo najua amenolewa na aweza shinda mashinano mahala popote duniani . Tena natoa shukran za dhati kwa waandalizi , nawaombea Mwenyezi Mungu awalipe duniani na akhera.
mwinyi ramadhani
0
0
Kwanza na wapongeza waandalizi wa mashindano haya ya kila mwaka , nikiwa mmoja niliechangia Hafidh Abdallah Yusuf , kuhudhuria mashindano hayo kama mfanya kazi wa kitengo cha utamaduni wa ubalozi wa Iran , Kenya , ni nani Imani kwamba huyu kijana akipewa nafasi mwakani atakuwa ni mwenye kupata namba za juu . Hata hivyo najua amenolewa na aweza shinda mashinano mahala popote duniani . Tena natoa shukran za dhati kwa waandalizi , nawaombea Mwenyezi Mungu awalipe duniani na akhera.
captcha