Mradi wa hivi karibuni wa kituo cha Kiislamu kinachojumuisha msikiti, shule na chuo cha kuhifadhi Qur’ani kimefunguliwa katika sherehe iliyohudhuriwa na Naibu Rais wa Jimbo la Jubaland Mohamoud Sayid Adan. Akizungumza katika uzinduzi wa mradi huo Sayid Adan ameishukuru Qatar kwa kuwasiadia wasiojiweza katika jamii kwa kuanzisha miradi yenye thamani.
Naye balozi wa Qatar nchini Somalia Hassan bin Hamza Hashem amesisitiza kuwa nchi yake inasimama pamoja na serikali ya Somalia katika miradi ya maendeleo huku akisisitiza kuhusu umuhimu wa uthabiti Somalia.
Kituo hicho za Kiislamu kinajumuisha shule ya msingi na upili, msikiti, uwanja wa michezo, ukumbu wa mikutano, kituo cha matibabu, madrassah ya kuhifadhi Qur’ani, maduka, na kisima.