IQNA

Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran

Waislamu wajitokeze kwa wingi katika maandamano ya Siku ya Quds Duniani

23:57 - June 29, 2016
Habari ID: 3470423
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya umuhimu wa Siku ya Kimataifa ya Quds na amewataka Waislamu hususan wananchi wa Iran kujitokeza kwa wingi katika maandamano ya siku hiyo Ijumaa wiki hii

Rais Rouhani amesema kuwa, mwaka huu kwa kuweko mshikamano na umoja zaidi ulimwengu utashuhudia maandamano makubwa zaidi katika Siku ya Kimataifa ya Quds nchini Iran na katika nchi nyingine ulimwenguni.

Amesema kuwa, wananchi wa Iran watajitokeza katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Quds kwa shabaha ya kuitikia wito wa Imam Ruhullah Khomeini MA muasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aliyeitangaza na kuianisha Ijumaa ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kuwa Siku ya Kimataifa ya Quds.

Rais Rouhani amesema kuwa, mbali na kuitikia wito wa Imam Khomeini MA wananchi wa Iran watajitokeza katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds kusaidia kupaza sauti ya kudhulumiwa ya wananchi wa Palestina ambao kwa takribani miaka 70 wametimuliwa katika nyumba zao na kulazimika kuwa wakimbizi.

Rais wa Iran amebainisha kuwa, Waislamu wataendelea na njia yao ya kuwaunga mkono wananchi wa Palestina kama ambavyo watadumisha harakati zao za kuikomboa Quds Tukufu kutoka mikononi mwa Wazayuni maghasibu.

Ijumaa Julai Mosi ni Siku ya Kimataifa ya Quds ambapo watu kutoka matabaka mbalimbali duniani wanatazamiwa kuandamana na kujumuika kwa lengo la kuonesha mfungamano wao na mapambano ya ukombozi wa Palestina sambamba na kuulani utawala wa Kizayuni wa Israel na waitifaki wake.

3511509


captcha