IQNA

Sayyid Hassan Nasrallah

Saudia inapuuza maslahi ya Wapalestina kwa kuhuisha uhusiano wake na utawala haramu wa Israel

0:29 - July 31, 2016
Habari ID: 3470484
Kiongozi wa harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amekosoa vikali safari ya maafisa wa ngazi za juu wa serikali ya Saudi Arabia katika utawala wa Kizayuni wa Israel wiki jana.
Sayyid Hassan Nasrallah ameongeza kuwa Saudia inahuisha uhusiano wake na utawala haramu wa Israel na kupuuza maslahi ya Wapalestina. Kiongozi wa Hizbullah amesema utawala wa Aal-Saud unatoa mfano mbaya kwa mataifa mengine na haswa ya Kiislamu katika kufufua uhusiano wake na utawala haramu wa Israel. Akizungumza Ijumaa kwa njia ya televisheni katika marasimu ya kukumbuka kifo cha Ahmad Zahri, mmoja wa makamanda wa harakati hiyo ya Kiislamu, Sayyid Nasrallah amesema sio jambo la mbali kwa utawala wa Riyadh katika hatua yake ya pili ya kufufua uhusiano wake na Israel, kutangaza kuutambua rasmi utawala huo bandia unaokalia kwa mabavu ardhi za Wapelestina.
Kauli ya Katibu Mkuu wa harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imekuja siku chache baada ya ujumbe wa ngazi za juu wa serikali ya Riyadh ukiongozwa na Jenerali Anwar Eshki, kamanda mkuu wa zamani wa Saudia kuutembelea utawala ghasibu wa Israel na kukutana na kufanya mazungumzo na wakuu wa utawala huo katili wakiwemo wabunge wa bunge la utawala huo, Knesset.
Eshki ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Kituo cha Mafunzo ya Kiistratejia na Sheria cha Mashariki ya Kati kilichoko Jeddah alikutana na kufanya mazungumzo na Dore Gold, Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Israel na Mshirikishi wa Masuala ya Harakati za Israel katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu Yoav Mordechai miongoni mwa maafisa wengine wa utawala huo wa Kizayuni.
Katika miezi ya hivi karibuni kumefuchuliwa mazungumzo ya siri baina ya maafisa wa ngazi za juu wa Saudia na Utawala wa Israel, jambo ambalo limeamsha hasira za Waislamu wengi duniani.
3460541
captcha