IQNA

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu

Ni kosa kubwa kudhani kuwa Marekani haiwezi kushindwa

16:14 - October 23, 2016
Habari ID: 3470629
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, dhana iliyotawala kwamba Marekani ni nchi isiyoweza kushindwa, ilikuwa ni kosa kubwa na kwamba makosa ya kujirudia ya Marekani katika eneo yameifanya ishidwe.
Ayatullah Sayyid Ali Khamenei aliyasema hayo jioni ya jana alipokutana na Rais Nicolás Maduro wa Venezuela ambapo sanjari na kuashiria kufeli kwa njama na siasa za Marekani katika eneo la magharibi mwa Asia, amegusia suala la kushushwa bei ya mafuta kuwa ni nyenzo ya kuzishinikiza nchi huru.

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameelezea utumiwaji wa silaha ya mafuta kwa ajili ya kuzitwisha matatizo nchi zinazojitegemea na kusema, wakati wa nyuma pindi baadhi ya nchi za Kiislamu zilipouwekea vikwazo vya mafuta utawala haramu wa Kizayuni, Wamagharibi, walitumia siasa ya mafuta kueneza makelele yao na kwamba kwa bahati mbaya nchi hizo hizo hii leo zimegeuka na kuwa waratibu wakubwa wa siasa za Marekani kupitia silaha ya mafuta.

Kiongozi Muadhamu ameashiria nafasi chanya ya Venezuela katika harakati dhidi ya uistikbari katika eneo la Amerika ya Latini kuwa ishara ya nafasi ya juu ya nchi hiyo sambamba na kumtaka rais wa taifa hilo atumie fursa ya uenyekiti wake wa Harakati ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande wowote NAM kufikia malengo yanayotarajiwa.
Ameongeza kuwa, Wamagharibi hawafurahishwi na harakati za jumuiya hiyo lakini akasisitiza kuwa, nchi huru lazima zisimame kukabiliana na njama hizo za Wamagharibi kwani kwa mwenendo huo kutaweza kufikiwa mustakbali mwema.

Kwa upande wake Rais Nicolás Maduro wa Venezuela sanjari na kupongeza muqawama wa taifa la Iran katika kukabiliana na adui Marekani amesema, katika hali ambayo raia wa taifa hili wanaishi kwa usalama na amani, akthari ya nchi nyingi za eneo na majirani zake wanaishi katika vita, tofauti na udhaifu.

Ameashiria kupungua kwa bei ya mafuta katika kipindi cha miaka miwili iliyopita na kuongeza kuwa, licha ya uingiliaji wa ubeberu wa Marekani na uadui mkubwa dhidi ya Venezuela, lakini raia wa nchi hiyo wamesimama kidete kukabiliana na vita vya kiuchumi na sasa wanaepukana taratibu na mgogoro huo.
3539912
captcha